Elimu

Majina ya Waliopata Mkopo HESLB 2024/2025

Majina ya waliopata mkopo HESLB 20242025

Majina ya Waliopata Mkopo HESLB 2024/2025: PDF Ya Orodha ya wanufaika wa mkopo HESLB Jinsi ya Kuangalia wanufaika Kupitia SIPA

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imeanza kutangaza orodha ya wanafunzi waliopangiwa mikopo kwa mwaka wa masomo 2024/2025. Orodha hii inajumuisha wanafunzi wapya wa shahada ya kwanza, shule ya Sheria kwa Vitendo, na wale wa shahada ya uzamili. Serikali imetenga TZS 787 bilioni kwa ajili ya kufadhili wanafunzi 245,799, wakiwemo zaidi ya wanafunzi 88,000 wa mwaka wa kwanza.

Jinsi ya Kuangalia Waliopata Mkopo Kupitia SIPA

Angalia hapa Matokeo

HESLB imerahisisha mchakato wa kuangalia mikopo kwa kutumia mfumo wa SIPA (Student’s Individual Permanent Account). Hii inawawezesha wanafunzi kupata taarifa zao za mikopo moja kwa moja kupitia akaunti zao bila kufika ofisi za HESLB.

Hatua za Kuangalia Mkopo Kupitia SIPA:
  1. Tembelea Tovuti Rasmi ya HESLB: Fungua www.heslb.go.tz.
  2. Ingia Kwenye Akaunti Yako ya SIPA: Tumia jina la mtumiaji na nywila uliyoitumia wakati wa kuomba mkopo.
  3. Angalia Taarifa Zako za Mkopo: Mara baada ya kuingia, utaweza kuona taarifa zote kuhusu mkopo wako na kiasi kilichotolewa.

Jinsi ya Kuangalia PDF Ya Majina ya Waliopata Mkopo Awamu ya Kwanza

Kwa wanafunzi wanaotaka kuangalia majina ya waliopata mikopo kupitia orodha ya PDF, HESLB pia hutoa majina ya wanufaika kwa awamu katika mfumo wa PDF. Orodha hizi mara nyingi hupatikana kwenye tovuti rasmi ya HESLB na zinaweza kupakuliwa na kuchapishwa.

Hatua za Kuangalia Majina Kupitia PDF:
  1. Tembelea Tovuti Rasmi ya HESLB: Nenda kwenye tovuti ya HESLB.
  2. Nenda Sehemu ya “Downloads” au “Announcements”: Katika ukurasa wa mbele, utaona sehemu maalum inayotangaza orodha ya waliopata mkopo.
  3. Pakua Orodha ya PDF: Bonyeza kiungo cha PDF kilicho na orodha ya awamu ya kwanza ya waliopata mkopo kwa mwaka 2024/2025.
  4. Tafuta Jina Lako: Baada ya kupakua faili ya PDF, unaweza kutafuta jina lako kwa kutumia Ctrl + F kisha andika jina lako au namba yako ya usajili.

Orodha ya Wanafunzi Walionufaika kwa 2024/2025

HESLB imepanga kutoa mikopo kwa jumla ya wanafunzi 245,799 mwaka huu, wakiwemo wanafunzi wapya 88,000 wa mwaka wa kwanza. Awamu ya pili ya majina ya waliopata mikopo inatarajiwa kutangazwa ndani ya wiki ijayo.

Kwa kutumia hatua hizi, wanafunzi wanaweza kwa urahisi kupata majina yao kwenye orodha ya waliopata mkopo HESLB kupitia akaunti za SIPA au kwa kupakua PDF inayotolewa na HESLB.

SOMA ZADI:Mwongozo wa Kuchagua Kozi Sahihi Vyuo Vikuu Tanzania

Leave a Comment